explain-icon

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake mara nyingi akipiga mswaki na akiamrisha watu kufanya hivyo, na kuna baadhi ya nyakati kumetiliwa mkazo, mfano; kupiga mswaki wakati wa kuamka usiku, kwani alikuwa rehema na amani ziwe juu yake akisukutua na kutakatisha kinywa chake kwa mswaki.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Mkazo wa sheria ya kupiga mswaki baada ya usingizi wa usiku, kwa sababu usingizi hupelekea mabadiliko ya harufu ya kinywa, na mswaki ndio kifaa cha kusafishia.
  • Mkazo wa sheria ya kupiga mswaki kila wakati wa mabadiliko ya harufu ya kinywa, kwa kuzingatia maana ya awali.
  • Sheria ya usafi kwa ujumla, na kwamba ni sehemu ya Sunna za Mtume rehema na amani ziwe juu yake, na ni katika adabu tukufu.
  • Kupiga mswaki katika kinywa chote kunajumuisha: Meno, fizi, na ulimi.
  • Mswaki ni kijiti kilichokatwa kutoka katika mti wa araki au mti mwingine, na hutumika kusafisha kinywa na meno, na huburudisha kinywa, na kuondoa harufu mbaya.