Anaeleza Abuu Musa Al Ash'ariy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: yakuwa yeye alikuja kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- naye akipiga mswaki kwa kutumia mti mbichi kwasababu husafisha kikamilifu na hausambaratiki mdomoni; ukakera, na hakika alikuwa kaweka mswaki juu ya ulimi wake, mpaka akawa kana kwamba anajitapisha.