Kutoka kwa bin Omari -Radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake-: Yakuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amekataza kunyoa kiduku.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake
Amekataza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kunyoa baadhi ya nywele za kichwa na kuacha baadhi.
Na katazo linawahusu watu wote, mwanaume mtoto mdogo na mkubwa pia, ama mwanamke hatakiwi kunyoa nywele za kichwa chake.
Katika Faida za Hadithi
Sheria ya Uislamu imetilia umuhimu wa muonekano wa kibinadamu.