Ameeleza Ukba bin Aamiri radhi za Allah ziwe juu yake yakwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alisema kumwambia: Usiku huu Mwenyezi Mungu kaniteremshia aya, hazijawahi kuonekana mfano wake katu -yaani katika kuomba kinga- nazo ni sura mbili za kinga: Suratu (Qul Auudhubirabbil falaq), na suratu (Qul Auudhubirabbin naas).