Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa hakuacha baada yake majaribu na mtihani wenye madhara makubwa kwa wanaume kuliko wanawake; Mwanamke akiwa ni katika familia yake huenda mume akamfuata mwanamke katika kwenda kinyume na sheria, na akiwa ni mwanamke wa kando yaweza kuwa ni kwa sababu ya kuchanganyika naye na kukaa naye faragha, na maovu mengine yanayoweza kusababishwa na hilo.