Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwamba laiti watu wangelijua yaliyomo katika Adhana na safu ya kwanza miongoni mwa fadhila na kheri na baraka, kisha wakakosa namna ya kutangulizana na nani awe bora kuliko mwingine ila kwa kupiga kura, basi wangelipiga kura, na lau wangelijua yaliyomo katika kuwahi swala mwanzo wa wakati wake basi wangelishindana kuyaendea, na laiti wangelijua kiwango cha thawabu katika kuiendea swala ya Ishaa na swala ya Alfajiri, basi kungekuwa kwepesi kuziendea hata kwa kutambaa kwa magoti kama anavyotembea mtoto mwanzo wa kukua kwake.