Alitahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kupita mbele ya mwenye kuswali swala ya faradhi au sunna, na kwamba lau angelijua mwenye kufanya hivyo kwa makusudi yale anayoyapata katika madhambi; basi angechagua kusimama arobaini; hilo ni bora zaidi kwake kuliko kupita mbele yake. Amesema Abuu Nasri mpokezi wa hadithi: Sijui alisema: Siku arobaini, au miezi au miaka.