Amehimiza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kula daku, nako ni kula mwisho wa usiku ili kujiandaa kwa ajili ya swaumu; kwa sababu ndani yake kuna baraka, na kheri nyingi, yakiwemo malipo na thawabu, na kusimama katika wakati wa mwisho kwa ajili ya kuomba dua, na kupata nguvu kwa ajili ya swaumu, na kupata uchangamfu kwa ajili yake, na kupunguza uzito wake.