Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa watu wataendelea kuwa katika kheri kwa muda wote watakaofanya haraka kufuturu ndani ya Ramadhani baada kuhakiki kuzama kwa Jua; na hii ni kwa sababu ya kutekeleza sunna, na kusimama katika mpaka wake.