Walikula daku baadhi ya Maswahaba pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake, kisha akasimama rehema na amani ziwe juu yake kwenda katika swala ya Alfajiri. Anasi akasema kumuuliza Zaidi bin Thabit radhi za Allah ziwe juu yake: Kulikuwa na kiwango cha muda gani baina ya adhana na kumaliza kula daku?. Akasema Zaidi radhi za Allah ziwe juu yake: Kiasi cha kusoma aya hamsini za kati na kati, si ndefu wala fupi, wala si kwa kisomo cha haraka wala cha taratibu.