explain-icon

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume Rehema na amani ziwe juu yake anapotaka kuingia mahali ambapo atakidhi haja yake hapo, haja ndogo au kubwa, anaomba kinga kwa Mwenyezi Mungu, na anajielekeza kwake amkinge na shari za mashetani wa kiume na wa kike, Na limetafsiriwa neno khubuthi na khabaaithi (Mashetani wa kiume na wa kike) kwa maana ya shari na najisi.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Sunna ya dua hii wakati wa kutaka kuingia msalani.
  • Viumbe wote ni wahitaji kwa Mola wao Mlezi katika kuzuia yenye kuwaudhi au kuwadhuru katika hali zao zote.