Waliletwa mateka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kutoka katika kabila la Hawazini, mara kukawa na mwanamke miongoni mwao akimtafuta mwanaye, kila akipata mtoto anamnyonyesha kwa sababu ya kudhurika kwake kwa wingi wa maziwa katika matiti yake, mara, akampata mwanaye katika mateka akamchukua, akamkumbatia tumboni kwake na akamnyonyesha, akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwaambia Maswahaba zake: Hivi mnadhani mwanamke huyu anaweza kumtupa mwanaye motoni? Tukasema: Kamwe, hawezi kumtuka kwa hiyari yake milele. Akasema: Basi Mwenyezi Mungu ana huruma zaidi kwa waja wake Waislamu kuliko mwanamke huyu kwa mtoto wake.