Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake yakwamba hakuna kundi la watu watakaokaa katika kikao kisha wakanyanyuka katika kikao hicho haliyakuwa hawajamtaja Mwenyezi Mungu ndani yake isipokuwa watanyanyuka katika mfano wa mzoga wa punda katika kunuka na uchafu; na hii ni kwa sababu walishughulika na mazungumzo wakaacha kumtaja Mwenyezi Mungu, na kikao hicho kwao kitakuwa ni masikitiko siku ya Kiyama na ni mapungufu na majuto kwao.