Mtume rehema na amani ziwe juu yake ameeleza nafasi ya wale wanaomkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na kwamba wao ni wa kipekee na wametangulia wengine katika kufikia daraja za juu katika Bustani za neema, na akawafananisha na mlima Jumdan ambao ni wa kipekee ukilinganisha na milima mingine.