explain-icon

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa mwenye kusimamia masilahi ya mwanamke aliyefiwa na mumewe na ikawa hakuna yeyote mwenye kusimamia mambo yake, na masikini muhitaji, na akawapa matumizi akitaraji malipo mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, basi mtu huyu katika malipo ni kama mpigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, na ni kama mwenye kusimama katika swala ya tahajudi asiyechoka, na mfungaji asiyefungua.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Himizo la kusaidizana na kuhurumiana na kutatua haja za watu madhaifu.
  • Ibada inakusanya kila amali njema, na miongoni mwa ibada ni kwenda haraka kuwasaidia wajane na masikini.
  • Amesema Bin Hubaira: Na makusudio yake hapa nikuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu humkusanyia thawabu za mfungaji na msimamaji usiku kwa ajili ya ibada na mpigana Jihadi kwa mpigo mmoja; na hii ni kwa sababu amesimama na mjane nafasi ya mume wake..., na akasimama upande wa masikini aliyeshindwa kujimudu mwenyewe, akatoa hiki kilichozidi katika matumizi yake, na akatoa sadaka kwa kuikandamiza nafsi yake, ndio maana manufaa yake yakawa sawa na swaumu na kisimamo cha usiku na Jihadi.