Zilikuwa talbiya (kuitika katika Hija) kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapotaka kuingia katika ibada ya Hija au Umra ni kusema: "Nimekuitikia ewe mola nimekuitikia" Kuitika kwa lazima kwako baada kukuitikia katika yale uliyotuita kwayo miongoni mwa ikhlasi na tauhidi na Hija na mengineyo, "Nimekuitikia, huna mshirika wako, nimekuitikia" wewe peke yako ndiye unayestahiki kuabudiwa huna mshirika wako katika uumbaji wako na uungu wako na majina yako na sifa zako, "hakika sifa njema" na shukurani na sifa "na neema" zinatoka kwako, na wewe ndiye mgawaji wake "ni zako" hugawanywa katika kila hali, "na ufalme" vile vile ni wako, "huna mshirika wako" wote ni wako wewe peke yako. Na alikuwa bin Omari radhi za Allah ziwe juu yao akizidisha katika hayo. "Labbaika wasa'daika" Nimekuitikia na utukufu ni wako, nifurahishe kwa furaha moja baada ya nyingine, "na heri iko mikononi mwako" yote, na ni kwa fadhila zako, "Nimekuitikia na shauku zote ziko kwako" na matakwa na maombi ninayaelekeza kwa yule ambaye heri iko mkononi mwake, "na matendo" ni kwa ajili yako, kwani wewe ndiye unayestahiki kuabudiwa.