Muislamu akitaka kufanya jambo katika mambo ambayo hayajulikani upande ulio sawa ndani yake, basi ni sheria kwake aswali swala ya Istikhaara (ya kuomba uamuzi) kiasi kwamba alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiwafundisha Maswahaba zake radhi za Allah ziwe juu yao swala hii kama anavyowafundisha sura ndani ya Qur'ani, anaswali rakaa mbili zisizokuwa za faradhi kisha anamuomba Mwenyezi Mungu kwa kusema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi ninakuomba uchaguzi" Kwa kuomba uniongoze katika jambo lenye kheri zaidi baina ya mambo mawili, na ninakuomba "Kupitia elimu yako", pana iliyozingira kila kitu, "na ninakutaka kupitia uwezo wako", wenye kutekelezeka kwani wewe hakikushindi chochote, "na ninakuomba katika fadhila zako" na wema wako "mtukufu" mpana; kwani kipawa chako ni fadhila kutoka kwako, na hakuna yeyote mwenye haki yake juu ya neema; "kwani wewe unaweza" juu ya kila kitu, na mimi ni dhaifu nisiyejiweza "na wala siwezi" jambo lolote isipokuwa kwa msaada kutoka kwako, "na" wewe "unajua" kwa elimu iliyokusanya na kuvizingira vyote vyenye kuonekana na visivyoonekana, na kwa kheri na shari, "na" mimi "sijui" chochote isipokuwa kwa taufiki yako na uongofu wako, "na wewe ni Mjuzi wa mambo ya ghaibu" wewe unaelimu isiyokuwa na mipaka, na uwezo wenye kutendeka, na hakuna kwa lolote katika hayo kwa yeyote asiyekuwa wewe awezaye kufanya hayo, ila yale uliyoyapanga kwake na ukamuwezesha. Kisha muislamu atamuomba Mola wake Mlezi, na atataja haja yake, kwa kusema: " Ewe Mola wangu" hakika mimi nimekabidhi jambo kangu kwako, basi "ikiwa unajua" katika elimu yako kuwa jambo hili "hapa atalitaja" kwa mfano kama kununua nyumba, au kununua kwangu gari hili, au kumuoa kwangu mwanamke huyu au mengineyo.... Ikiwa jambo hili lilikwishatangulia katika elimu yako yakuwa ndani yake kuna "kheri kwangu katika dini yangu" ambayo ndiyo ngome ya jambo langu, "na maisha yangu" katika dunia yangu "na mwisho wa jambo langu" na hatima ya jambo langu, au alisema: "haraka ya jambo langu na kuchelewa kwake" katika dunia na Akhera; "liwezeshe" na uliandae na ulitimize "kwangu", na ulirahisishe "na ulifanye kuwa jepesi kwangu" "kisha libariki" na ukithirishe kheri "ndani yake kwangu", "na ikiwa unajua" ewe Allah "kuwa jambo hili" nililokuamba uamuzi kwalo "ni shari kwangu katika dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu -au alisema katika haraka ya jambo langu na kuchelewa kwake, basi liepusha nami na uniepushe nalo, na unikadirie kheri mahala popote itakapokuwa, kisha niridhishe nayo" na kwa hukumu zako zote ninazozipenda na ninazozichukia.