Aliamrisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwapiga vita makafiri, na kutumia juhudi katika kukabiliana nao kwa kila nyenzo kwa kadri iwezekanavyo, ili neno la Mwenyezi Mungu liwe juu, na miongoni mwake: Kwanza: Kutoa mali katika kuwapiga vita; ikiwemo kununua silaha, na kutoa mahitaji kwa wapiganaji, na mfano wake. Pili: Kutoka kwa nafsi na mwili ili kukabiliana nao na kuwazuia. Tatu: Kwa kuwalingania waingie katika dini hii kwa ulimi, na kuwasimamishia hoja juu yao, na kuwakemea na kuwajibu hoja zao.