Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa peponi kuna daraja na vituo mia moja, na masafa yaliyopo kati ya daraja mbili ni kama masafa kati ya mbingu na ardhi, na Pepo ya juu zaidi miogongoni mwa Pepo hizi ni Pepo ya Firdausi, na ndani yake ndiko inapochimbuka mito yote minne ya Pepo, na juu ya Firdausi ndiko inakokuwa Arshi; mkimuomba Mwenyezi Mungu basi muombeni Firdausi; kwani ndiyo iko juu ya Pepo zote.