Alisimama Mtume rehema na amani ziwe juu yake mbele za watu waliokaa miongoni mwa Maswahaba zake akawauliza, je nisikuelezeni na nikumbusheni ni nani mbora wenu na ni nani muovu wenu? Wote hawakuzungumza na wala hawakujibu chochote, kwa kuhofia kubainishwa mbora wao na muovu wao na wakahofia fedheha wakanyamaza. Mtume rehema na amani ziwe juu yake akarudia swali mara tatu, akajibu mtu mmoja miongoni mwao: Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, tueleze mbora wetu na muovu wetu. Mtume rehema na amani ziwe juu yake akawabainishia: Kuwa mbora wenu ni yule inayesubiriwa na kutarajiwa heri yake na ihisani yake na wema wake, na kuaminiwa kutowepo shari yake kusiogopwe uadui wake na uonevu wake na dhuluma yake, na kuwa muovu wenu ni yule asiyetarajiwa wala kusubiriwa wala kutamaniwa kupatikana heri yake na ihisani yake na wema wake, na haiaminiwi shari yake, bali unahofiwa uadui wake na uonevu wake na dhuluma yake.