explain-icon

Ufafanuzi

Mtume rehema na amani ziwe juu yake anamhimiza muislamu kumsalimia ndugu yake muislamu kila anapokutana naye, hata kama wakiwa wanatembea pamoja na kikawatenganisha chochote, kama mti au ukuta au jiwe kubwa, kisha akakutana naye baada ya hapo basi amsalimie kwa mara nyingine.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Ni sunna kusambaza salam, na irudiwerudiwe kila hali inapobadilika.
  • Pupa yake kubwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika kusambaza sunna ya salam na kukithirisha; kwakuwa ndani yake kuna kuleta mapenzi na kuzoeana kati ya waislamu.
  • Salaam ni kusema: "Assalaam alaikum" Amani iwe nanyi, au "Assalaam alaikum warahmatullaahi wabarakaatuh", Amani ya Mwenyezi Mungu iwe nanyi na rehema zake na baraka zake", hii ni tofauti na kupeana mkono kunakotokea mara ya kwanza wakati wa kukutana.
  • Salam ni dua, na waislamu wanahaja kubwa ya kuombeana wao kwa wao hata kama litajirudiarudia hilo.