explain-icon

Ufafanuzi

Amekataza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kupigwa mtu yeyote zaidi ya viboko kumi isipokuwa katika maasi, na pia hakuna maelekezo yoyote yaliyokuja katika sheria kueleza idadi maalumu ya viboko au kipigo au adhabu maalumu, na makusudio yake haizidishwi katika kipigo cha kuadabisha zaidi ya viboko kumi, kama kumpiga mke au mtoto.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Mipaka ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliyoiamrisha au aliyoikataza inaadhabu zinazokomesha hayo, ima zimepangwa katika sheria, au zinarudi kukadiriwa kwake katika masilahi anayoyaona hakimu.
  • Kutia adabu kunakuwa kwa kiasi kidogo, kwa kiasi cha kuelekeza na kuhofisha, kusizidishwe zaidi ya viboko kumi ikibidi kufanya hivyo, na kilichobora zaidi ni kuwaadabisha pasina kuwapiga, bali kwa kuwaelekeza, na kuwafundisha, na kuwaongoza, na kuwatia hamasa, hilo huleta msukumo mkubwa wa kukubali na upole katika kujifunza, na hali katika nafasi hii hutofautiana sana, inapasa mtu afanye kinachofaa.