Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: Watu wa aina tatu mimi ndiye nitakayepambana nao siku ya Kiyama, na nitakayekuwa mgomvi wake basi nitapambana naye na kumshinda: Wa kwanza: Atakayetoa kiapo na akaapa kwa jina la Mwenyezi Mungu, na akachukua ahadi kisha akaitengua na kufanya hiana. Wa pili: Atakayemuuza mtu huru kwa kumfanya kuwa mtumwa na akala thamani yake na akakitumia kiwango cha pesa aliyopata. Wa tatu: Atakayemuajiri muajiriwa katika kazi, akamtimizia kazi yake na hakumpa thamani ya kazi yake.