Alikuja mtu mmoja kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wasemaje endapo atakuja mtu akataka kuchukua mali yangu? Akasema: Hutakiwi kujisalimilisha kwake na ukampatia mali yako, akasema: Wasemaje akipigana nami? Akasema: Inafaa kwako kupigana naye, akasema: Wasemaje endapo ataniuwa? Akasema: Basi wewe utakuwa shahidi, akasema: Wasemaje endapo nikimuuwa? Akasema: Basi yeye atastahiki kuadhibiwa motoni siku ya Kiyama.