Alikuja mama Kaisi binti Mihswan radhi za Allah ziwe juu yake kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiwa na mtoto wake hajaanza kula chakula kutokana na udogo wa umri wake, Mtume rehema na amani ziwe juu yake akamkalisha katika mapaja yake, mtoto akakojoa katika nguo yake rehema na amani ziwe juu yake, akaomba maji, na akanyunyiza katika nguo yake na wala hakuiosha.