Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayeshikamana na nembo za dini za wazi akaswali mfano wa swala yetu, na akaelekea upande wa Ka'aba Kibla yetu, na akala kichinjwa chetu kwa kuamini kuwa ni halali; basi huyu ndio Muislamu ambaye anadhima ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na ahadi yake, msitengue amani ya Mwenyezi Mungu na ahadi yake ndani yake.