explain-icon

Ufafanuzi

Alibainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa mtu hufanana na rafiki na jamaa yake wa dhati katika nyenendo na tabia zake, na urafiki huathiri maadili, tabia na matendo, na kwa ajili hiyo alielekeza vyema katika uchaguzi wa rafiki. Kwa sababu atamuongoza rafiki yake katika imani na uongofu na kheri, na atakuwa ni msaada kwa rafiki yake.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Amri ya kusuhubiana na wema na kuwachambua, na katazo la kusuhubiana na watu wabaya.
  • Ametajwa rafiki badala ya ndugu; Kwa sababu wewe ndiye unayemchagua rafiki, lakini ndugu na jamaa, huna chaguo.
  • Kumchukua mtu kuwa rafiki lazima kuanze na kutafakari.
  • Mtu huiimarisha dini yake kwa kusuhubiana na waumini na huidhoofisha kusuhubiana na watu waovu.