Aliulizwa Hafswa mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake: Kilikuwa vipi kisomo cha Qur'ani cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake? Akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi mfano wake, akaambiwa: Tueleze. Amesema Naafii: Akatusomea Abuu Mulaika kisomo alichotulizana ndani yake; ili kielezee na kikaribiane na kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasoma: "Alhamdulillaahi Rabbil Aalamiin" kisha akakata kisomo, "Al Rahmaanir Rahiim", kisha akakata kisomo, "Maaliki yaumid diin".