Kutoka kwa Abuu Mulaika: Kutoka kwa baadhi ya wake za Mtume rehema na amani ziwe juu yake, amesema: Abuu Aamir, amesema Naafii: Nafikiri ni Hafswa -Yakuwa aliulizwa kuhusu kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi, akasema: Akaambiwa hebu tueleze. Akasema: Akasoma kisomo cha taratibu, akasema Abuu Aamiri: Akasema Naafii: Akatusimulia Abuu Mulaika: "Alhamdulillaah Rabbil-Aalamiin" [Al-Faatiha: 1] Kisha akakata "Al Rahmaanir Rahiim" [Faatiha:3] kisha akakata "Maaliki yaumid diin". Sahihi - Imepokelewa na Ahmad
explain-icon

Ufafanuzi

Aliulizwa Hafswa mama wa waumini radhi za Allah ziwe juu yake: Kilikuwa vipi kisomo cha Qur'ani cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake? Akasema: Hakika nyinyi hamkiwezi mfano wake, akaambiwa: Tueleze. Amesema Naafii: Akatusomea Abuu Mulaika kisomo alichotulizana ndani yake; ili kielezee na kikaribiane na kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akasoma: "Alhamdulillaahi Rabbil Aalamiin" kisha akakata kisomo, "Al Rahmaanir Rahiim", kisha akakata kisomo, "Maaliki yaumid diin".

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Kumebainishwa muongozo wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika kusoma Qur'ani.
  • Kufanya kwa vitendo ili kubainisha namna ya kisomo cha Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
  • Sheria ya kwenda taratibu katika kuisoma Qur'ani, hilo huleta msukumo wa kuizingatia.
  • Kuitilia maanani Qur'ani wema waliotangulia, na matendo ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
  • Umuhimu wa kujua kanuni za kuisoma Qur'ani (Tajwidi) na elimu za Qur'ani.