Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba atakayejifunza elimu ya kisheria ambayo asili yake ni kutafutwa radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu, hajifunzi isipokuwa apate heshima na starehe za kidunia miongoni mwa mali au cheo, basi hatoipata harufu ya Pepo siku ya Kiyama.