Kutoka kwa Abuu Shuraihi radhi za Allah ziwe juu yake yakuwa Mtume rehema na amani za Allah ziwe juu yake amesema: "Wallahi hawezi kuamini, Wallahi hawezi kuamini, Wallahi hawezi kuamini", wakasema: Na ni nani huyo ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: "Ambaye hapati amani jirani yake kwa kero zake". Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
explain-icon

Ufafanuzi

Aliapa Mtume rehema na amani ziwe juu yake na akasisitiza kiapo chake mara tatu, akasema: Wallahi hawezi kuamini, Wallahi hawezi kuamini, Wallahi hawezi kuamini, Maswahaba wakamuuliza: Na ni nani ambaye hawezi kuamini ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Akasema: Ambaye jirani anahofia usaliti wake na dhulma zake na shari zake.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Kukanushwa imani kwa yule ambaye jirani yake hapati amani kutokana na dhulma zake na shari zake hili linaonyesha kuwa ni katika madhambi makubwa, na kwamba mfanyaji wake anaupungufu wa imani.
  • Himizo la msisitizo juu ya kumtendea wema jirani na kuacha kumuudhi kwa kauli au kitendo.