Imepokewa kutoka kwa Anas bin Maliki -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake: "Msaidie ndugu yako akiwa amedhulumu au kudhulumiwa", Akasema mtu mmoja: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, unaonaje ikiwa ndugu yangu kadhulumu, vipi nitamsaidia? Akasema: "Unamuhama au unamzuia asifanye dhulma, kwa kufanya hivyo ndiyo kumnusuru". Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
explain-icon

Ufafanuzi

Mtume rehema na amani ziwe juu yake amemuamrisha Muislamu kumsadia ndugu yake Muislamu sawa sawa awe kadhulumu au kadhulumiwa, mtu mmoja akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nimnusuru atakapokuwa emedhulumiwa kwa kumuondolea dhuluma, wasemaje ikiwa kadhulumu nitamsaidia vipi? Akasema: Utamzuia, na kumshika mkono na umkinge na umzuie na dhuluma; kwa kufanya hivyo ndiko kumnusuru dhidi ya Shetani wake na nafsi yake yenye kuamrisha maovu.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Hapa kuna tahadhari juu ya haki miongoni mwa haki za udugu wa kiimani baina ya Waislamu.
  • Kumzuia dhalimu, na kumkataza dhidi ya dhuluma.
  • Uislamu unakwenda kinyume na uelewa wa zama za ujinga, kiasi ambacho walikuwa wakisaidizana sawa sawa wawe wamedhulumiwa wao wamemdhulumu mwingine.