Anaapa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa hakuna atayemsikia katika umma huu, Myahudi au Mkristo au mwingine yeyote utakayemfikia ujumbe wa Mtume -sala na amani ziwe juu yake- kisha akafa na hakumuamini isipokuwa atakuwa miongoni mwa watu wa motoni ataishi humo milele daima.