Kutoka kwa Ally radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akitusomesha Qur'ani katika kila hali madamu hana janaba.
Ni nzuri (Hasan) - Imepokelewa na Abu Daud, Tirmidhiy, Nasai, Ibn Majah na Ahmad
Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiwafundisha Maswahaba zake Qur'ani na akiwasomesha yeye mwenyewe katika hali zote madam hajawa katika hali ya janaba litokanalo na tendo la ndoa kwa wakeze.
Katika Faida za Hadithi
Kutofaa kusoma Qur'ani kwa mwenye janaba mpaka aoge.