Alibainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa moja ya aina kubwa ya jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na yenye manufaa makubwa ni neno la uadilifu na ukweli mbele ya mtawala au mfalme dhalimu, kwa sababu ni kuifanyia kazi sheria ya kuamrisha mema na kukataza maovu, iwe kwa maneno au maandishi au vitendo, au kitu chochote kile, ili kuleta manufaa na kuzuia maovu.