Walikuwa maswahaba wakikumbushana fitina ya masihi dajali na wakiogopeshana juu yake, akawaeleza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa kuna jambo la haramu analowaogopea kuliko hata hofu ya fitina ya masihi dajali, nayo ni shirki katika nia na makusudio ambayo haionekani kwa watu, kisha akalifasiri hilo kwa kuyafanya vizuri matendo ambayo hutafutiwa kwayo radhi za Mwenyezi Mungu kwaajili ya kuwaonyesha watu.