explain-icon

Ufafanuzi

Ameeleza Aisha radhi za Allah ziwe juu yake yakuwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake alikuwa akidumu na swala za sunna ndani ya nyumba yake na wala haziachi: Rakaa nne kwa salamu mbili kabla ya swala ya Adhuhuri, na rakaa mbili kabla ya swala ya Alfajiri.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Sunna ya kuzihifadhi na kudumu na rakaa nne kabla ya swala ya Adhuhuri, na rakaa mbili kabla ya swala ya Alfajiri.
  • Kilicho bora ni swala za sunna ziswaliwe nyumbani, na ndivyo alivyoeleza Aisha radhi za Allah ziwe juu yake.