Aliomba Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema: Ewe Mola wangu, hakika mimi ni mwanadamu, hivyo basi, muumini yeyote niliyemuudhi au kumtukana au kumshutumu, au kumlaani, na nikamuombea kufukuzwa katika rehema yako, au nilimpiga mjeledi au kipigo chochote, basi lifanye hilo kwake kuwa ni utakaso na ibada na twahara na kafara na rehema utakayomhurumia kwayo.