Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba muumini huendelea kuwa katika nafasi pana ya matendo mema, na kutaraji rehema ya Mwenyezi Mungu na msamaha na maghufira yake, mpaka atakapouwa mtu aliyeharamishwa kuuawa basi amali zake zitakuwa nyembamba kwake; kwa sababu hazitoshelezi kulipa mauaji na dhambi lake kubwa.