Alifariki mama Sa'di bin Ubada radhi za Allah ziwe juu yake, akamuuliza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ni aina ipi bora ya sadaka ili aitoe kwa niaba ya mama yake? Akamueleza rehema na amani ziwe juu yake: Kuwa sadaka bora ni maji, akachimba kisima na akakifanya kuwa sadaka kwa ajili ya mama yake.