Alisoma Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa sura ya wattin wazzaitun ndani ya rakaa ya kwanza katika swala ya ishaa; kwasababu yeye alikuwa safarini, na safari ni lazima izingatiwe kufanya wepesi (tahfifu) kwasababu ya shida na matatizo yake, na pamoja nakuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa msafiri, lakini hakuyaacha yale yanayochochea kupatikana kwa utulivu na kuhudhurisha moyo wakati wa kusikiliza Qur'ani, nako ni kupendezesha sauti katika kisomo cha swala.