Eneo la Qubaa ambapo umejengwa hapo msikiti wa kwanza katika uislamu ni kijiji kilichopo karibu na kituo cha Madina tokea pande za kusini mashariki ya mji wa Madina,akawa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anautembelea msikiti wa Qubaa akiwa katika kipando na akiwa kwa miguu, na aliposema kila juma mosi: makusudio nikuwa alikuwa akitenga baadhi ya siku kwaajili ya ziara, na hekima ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake kuja Qubaa siku ya juma mosi katika kila wiki, ilikuwa ni ajili ya kuunga udugu na maanswari na kujua hali zao na hali ya yule aliyechelewa kuipata swala ya ijumaa pamoja naye,na hii ndio siri ya kuichagua ziara katika sikuya juma mosi.