Alimuuliza Omar bin Khattwab -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ikiwa mmoja wao atapatwa na janaba mwanzoni mwa usiku, kwa kumuingilia mke wake hata kama hakumwaga au akajiotea, Je alale nayeye akiwa na janaba? Akawaruhusu -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa hilo, kwa kupunguza hadathi (uchafu) huu mkubwa kwa udhu wa kisheria; na hapo haina tatizo mtu kulala na janaba.