Kutoka kwa Ummu Salama mama wa waumini mke wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Atakayeandaa mnyama kwa ajili ya kuchinja, na ukaandama mwandamo wa mwezi Dhul Hija, basi asipunguze chochote katika nywele zake wala kucha zake mpaka atakapochinja mnyama wake wa Udh-hiya" Sahihi - Imepokelewa Imamu Muslim
explain-icon

Ufafanuzi

Amemuamrisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake atakayetaka kuchinja Udh-hiya asipunguze chochote katika nywele za kichwa chake au kwapa yake au sharubu zake au zinginezo, wala sehemu ya kucha za mikono yake wala miguu yake utakapoonekana mwandamo wa Dhul-Hija mpaka atakapochinja.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Atakayenuia kuchinja baada ya kuingia siku kumi basi aanze kujizuia kulikoelezwa kwanzia wakati aliponuia mpaka atakapochinja.
  • Asipochinja katika siku ya kwanza, ataendelea kujizuia mpaka atakapochinja katika siku yoyote miongoni mwa siku za kubanika nyama.