Anatueleza Abdillahi bin Abbasi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- katika nukuu hii kuwa kiwango cha asilimia ya mbingu saba na ardhi saba pamoja na ukubwa wake katika kiganja cha Ar-Rahmaani -Mwingi wa Rehema-, ni kama kiwango cha punje ndogo ya ulezi katika kiganja cha mmoja wetu, na hii ni kufananisha kiwango kwa kiwango, na si kufananisha kiganja kwa kiganja; kwasababu Mwenyezi Mungu sifa zake hazifanani na kitu chochote kama ambavyo dhati yake haifanani na chochote.