Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa Manabii wote Mwenyezi Mungu aliwapa nguvu na akawapa alama na miujiza iliyo nje na kawaida ya watu, watakayoitumia kama ushahidi juu ya unabii wao na kumpelekea kuamini atakayeishuhudia kwa kuwasadikisha, na kwamba yeye ameshindwa katika changamoto hiyo, kiasi kwamba hawezi kuizuia yeye mwenyewe binafsi, lakini anaweza kupinga akakaidi. Bali yeye rehema na amani ziwe juu yake alama yake na muujiza wake ni Qur'ani aliyomteremshia Mwenyezi Mungu kwa Wahyi; kwa namna ilivyokusanya miujiza ya wazi tena endelevu kwa wingi wa faida zake na kuenea kwa manufaa yake, kwa kukusanya kwake ujumbe na hoja na habari za yale yatakayotokea, manufaa yake yakamuenea aliyepo na asiyekuwepo na aliyepatikana na atakayepatikana, kisha akasema: Basi ninataraji kuwa na wafuasi wengi zaidi yao siku ya Kiyama.