explain-icon

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa katika haki za Muislamu kwa ndugu yake Muislamu ni kumlisha mwenye njaa na kumtembelea mgonjwa, na kumuacha huru mateka.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Himizo la Waislamu kusaidizana.
  • Himizo la kumlisha chakula mwenye njaa na uhitaji, huyu imeamrishwa kumlisha.
  • Sheria ya kumtembelea mgonjwa; ili kumpa faraja, na kumuombea dua na kupata malipo, na mengineyo.
  • Kufanya pupa kumwacha huru mateka aliyetekwa na makafiri, na hiyo ima kwa kulipa gharama inayohitajika ili kumuondoa mikononi mwao, au kwa kubadilisha nao na mateka wa kikafiri, yaani: Kwa njia ya kubadilishana.