Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Akisema: "Haijabakia katika utume isipokuwa viashiria vya habari njema" wakasema: ni vipi hivyo viashiria? Akasema: "Ni ndoto njema".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anaashiria Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa ndoto njema ndio viashiria, nazo ndiyo athari za utume zilizobakia baada ya kukatika kwa wahyi, na hayajabakia yanayoweza kutumika kujua mambo yatakayotokea isipokuwa ndoto njema.