Anawakemea bin Abbasi watu miongoni mwa wale waliohudhuria kikao chake katika watu wa kawaida wanaopatwa na hofu pale wanaposikia chochote katika hadithi za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuhusu sifa, na wanatikisika kama ishara ya kulipinga hilo, haijapatikana kwao imani ya wajibu kwa yale yaliyothibiti toka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na wakajua maana yake kutoka ndani ya Qur'ani ambayo muumini hawezi kuwa na shaka, na baadhi yao huzichukulia katika maana isiyokuwa yake aliyoitaka Mwenyezi Mungu wakaangamia kwa hilo.