explain-icon

Ufafanuzi

Anaeleza Baraa bin Azibi radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake ya kwamba hajawahi kumuona yeyote nywele za kichwa chake ni ndefu zimefika katika mabega yake, na anayevaa kikoi na shuka jeusi na lenye mistari myekundu zuri kuliko Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake, na kwamba miongoni mwa sifa zake za kimaumbile ni kwamba mabega yake yalikuwa mbali mbali, mwenye kifua kipana, na alikuwa na kimo cha kati na kati, kati mrefu na mfupi.

explain-icon

Katika Faida za Hadithi

  • Hapa kumebainishwa baadhi ya sifa nzuri za Mtume- rehema na amani ziwe juu yake- katika muonekano, kama uzuri wa nywele na upana wa kifua, na uzuri wa kimo, na mengineyo.
  • Mapenzi ya Maswahaba watukufu kwa Mtume- rehema na amani ziwe juu yake-, kiasi kwamba mpaka walikuwa wakielezea na wakiwanukulia waliokuja baada yao miongoni mwa muonekano wake na sifa zake za kimwili na za kimaana (zisizoonekana).