Haya(Aibu) ni sifa iliyoko katika nafsi inayomsukuma mtu kufanya mazuri au yanayopendeza, na kuacha yanayochafua na kuharibu, na ndio maana haiji isipokuwa kwa kheri, na sababu ya kuja kwa hadithi hii nikuwa mtu mmoja alikuwa akimnasihi ndugu yake kuhusu haya, na akimkataza kuhusu haya, Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akasema kumwambia maneno haya.